NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA
JUMLA ya Mashauri saba ya kesi za mauaji yameanza kusikilizwa
katika Mahakama ya Hakimu mkazi wilaya ya Kigoma mkoani hapa na
Jaji mfawidhi mahakama kuu Kanda ya Tabora
Sam Rumanyika kwa lengo la kuongeza ufanisi na kuwapunguzia gharama
wateja wao.
Akitoa kauli hiyo leo kwenye viwanja vya mahakama hiyo katika
ufunguzi wa usikilizwaji wa kesi hizo, Naibu
Msajili Mahakama kanda ya tabora Shamillah Sarwatt alisema wanafanya
kazi ya kusikiliza mashauri ya kesi za
mauaji ndani ya muda katika maeneo
husika ili, kutoa haki kwa wateja.
Alifafanua kuwa, kazi ya mahakama ni kusikiliza mashauri na
kutoa haki kwa wote na kwa wakati hasa katika shauri la mauaji nia kumwezesha mteja asitumie gharama kubwa
kutafuta haki hizo, ambapo serikali imejiwekea utaratibu huo, ili kuongeza
ufanisi kwa wadau wa idara ya sheria.
Alieleza kuwa, miongoni mwa mashauri ya mauaji hayo awali zilishasikilizwa katika vipindi tofauti
tofauti hususani mashauri ya mwaka 2007 na mwaka 2012 ambapo zilishafikishwa
katika mahakama ya rufani hali inayoilazimu mahakama ya kanda kuwafuata wateja
maeneo husika ili kutoa haki kwa wote.
Alianisha kuwa kesi tano zitasikilizwa leo katika mahakama ya
hakimu mkazi wilaya ya kigoma na mashauri mawili yatasikilizwa katika mahakama
ya wilaya ya Kibondo ambapo wateja watatumia fursa hiyo katika kupata haki zao
za msingi kabla ya kutolewa hukumu husika.
Awali kabla ya
kusikilizwa ka mashauri hayo Jaji Sam
Rumanyika alikagua gwaride la Kikosi cha Askari wa kutuliza ghasia( FFU)
hatimaye mchakato wa usikilizaji wa kesi tano za mauwaji dhidi ya walengwa
zilianzwa kusikilizwa .
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: