CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) KIGOMA WATAKA MADIWANI WALIO WAGOMBANA KUFIKISHWA KWENYE KAMATI YA MAADILI

MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA

IMEELEZWA kuwa, Madiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM )Wawachukuliwe hatua za kinidhamu kwa kupeleka malalamiko katika kamati ya maadili ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, ili kuwakumbusha wajibu wao, madiwani waliopigana katika Ukumbi wa Manispaa ya Kigoma ujiji katika Kikao cha baraza la madiwaniti hivi karibuni.

Hayo yalisemwa jana katika ukumbi wa kizoto Manispaa ya Kigoma  ujiji  katika Kongamano la Wanachama wa  ccm wilayani  kigoma Mjini na Viongozi wa Chama  katika sherehe  ya miaka 40 ya CCM, alisema Kitendo hicho cha Madiwani kupigana katika jengo la Halmashauri hakipaswi kufumbiwa macho ni lazima Wachukuliwe hatua za kinidhamu ili iwe fundisho kwa wengine.

Akithibitisha hilo Mwenyekiti wa Chama hicho kigoma Dkt, Aman Kabourou alisema  kitendo cha diwani Revocatusi Chipando (BABA REVO) kumtuhumu  Diwani wa kata ya Kibirizi Rashid Luhomvya kwa madai kuwa diwani  mwenzake huyo wa chama hicho  ni mwizi wa miradi ya umma,
Alisema tabia zinazo endelea katika Manispaa hiyo kwa kushirikiana na  Viongozi wa halmashauri kuiba fedha za miradi ya maendeleo kwa kuahidiana kugawana lakini pindi wanapo hindwa kutimiza ahadi zao wanapigana katika kikao cha madwiani  kwa kuwatumia madiwani wasio na haya akiwemo Baba Revo.

" Manispaa ni jengo tukufu liheshimiwe na kila mtu, suala la  madiwani kupigana katika halmashauri lichukuliwe hatua za kinidhamu hatuwezi kuvumilia sisi kama Chama kinacho tawala na Serikali iliyopo madarakani, lazima tuhakikishe sula hili linashugulikiwa , maendeleo hayaji  madiwani wataendelea na malumbano",alisema Kabourou.
Alisema Wananchi wa Manispaa ya Kigoma Walifanya Makosa kuikabidhi halmashauri  chama ambacho  kinahitaji kujijenga (ACT) kwa kuwa  hakiwezi kushughulikia kero za wananchi kwa lengo la kuchochea maendeleo na uchaguzi  ujao wasirudie makosa waliyoyafanya leo.

Kwa upande Wake katibu wa Mkoa wa Kigoma Naomi Kapambala alisema Suala la CCM kupoteza jimbo la Kigoma mjini pamoja na kata zote ni usaliti uliofanywa na baadhi ya Wanachama wa CCM waliokisaliti Chama kwa kupewa rushwa hali inayowatesa raia ambao walipiga kura kwa njia ya rushwa.

Alisema katika kuiunda  CCM mpya na Serikali mpya watahakikisha wanawaondoa  wasaliti wa chama  hicho waliopelekea  kushindwa katika chaguzi zake na kuonya mamluki kuwa ccm ndio mtatuzi wa kero za wananchi kwa ujumla.

Aidha Wanachama kupitia  uchaguzi wa viongozi wa Chama  2017 wahakikishe wanatenda haki kwa kuchagua viongozi wenye sifa bila kujali masuala ya rushwa yanayo sababisha kuua Chama kwa kuwa, baadhi ya viongozi  wanatumiwa na Vyama vya upinzani ili,kukiangusha chama hicho.

Alisema wakibaini kiongozi ameshinda kwa kutoa rushwa watamuondoa , hakuna kiongozi anae shinda kwa misingi ya rushwa na kukitumikia Chama kwa uzalendo na uadilifu  kwa kuwa,wengi wao ndio wale wasariti  wa chama wakipewa pesa wako radhi kukiuza chama na kudai  Viongozi wa aina hiyo hawaitajiki ccm.

Kwa upande wake katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kigoma mjini Zuberi Mabiye alisema  kitendo cha  Diwani wa kata ya Kibirizi Ruhovya Yunusi  na diwadi wa kata ya Mwanga Kasikazini Revocatusi  Chipando (Baba Revo ) si cha ungwana kwa raia na kama wananyimana miradi watumie kamati za huduma za kijamii kujadili hayo.

0 comments: