AL: ISRAEL NI MKIUKAJI MKUBWA WA HAKI ZA BINADAMU

Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeutuhumu utawala haramu wa Israel kwa kuhusika na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadmau Palestina.
Katika taarifa yake ya kila mwaka ya 'Hali ya Haki za Binadamu Duniani', Amnesty International imesema Israel inahusika na mauaji ya kiholela ya Waplestina, kuwakamata na kuwaweka kizuizini bila sababu, utesaji wafungwa wa Kipalestina na vitendo vingine vingi vya ukiukwaji wa haki za binaadamu. Taarifa hiyo imesema Israel inakiuka sheria za kimataifa katika vitendo vyake vya kidhalimu dhidi ya Wapalestina. Amnesty imesema wanajeshi wa Israel wanawatesa wafungwa wakiwemo watoto. Hali kadhalika katika kipindi cha mwaka mmoja wanajeshi wa Israel wamehusika na mauaji ya idadi kubwa ya Wapalestina.
Nyumba za Wapalestina zilizoharibiwa na jeshi la Israel katika Ukanda wa Ghaza
Shirika hilo la kutetea haki za binadamu limelaani hatua ya Israel kuendeleza mzingiro ulio kinyume cha sheria dhidi ya Ukanda wa Ghaza kwa muda wa mwaka wa 10 sasa. Amnesty pia imeulaani utawala haramu wa Israel kwa kubomoa nyumba za Wapalestina katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu. Ripoti hiyo imesema katika Ukingo wa Magharibi na Quds Mashariki, wakuu wa Israel walibomoa nyumba 1,089 za Wapalestina na kuwafurusha watu 1,593 kutoka nyumba zao mwaka jana.
Askari wa utawala haramu wa Israel wameua Wapalestina 280 tokea Intifadah au mwamko wa pili uanze dhidi ya Israel Oktoba mwaka 2015. Aidha hivi sasa Wapalestina zaidi ya 6,500 wanashikiliwa katika jela za kuogofya za utawala huo wanakoshikiliwa pasina kufunguliwa mashtaka.

0 comments: