AFGHANISTAN: MAMIA YA WANAWAKE WATUMWA MWA NGONO NA KUNDI LA ISIS NCHINI HUMO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:14 AM
Mkuu wa Taasisi ya 'Uadilifu kwa ajili ya
Wote' nchini Afghanistan amesema kuwa, kundi la kigaidi na ukufurishaji
la Daesh limewafanya watumwa wa ngono zaidi ya wanawake 100 katika miji
tofauti ya mkoa wa Nangarhar nchini humo ndani ya kipindi cha miaka
miwili iliyopita.
Hamideh Wardak, ameyasema hayo katika kikao na waandishi wa
habari mjini Kabul, mji mkuu wa Afghanistan na kuongeza kuwa, wanawake
hao walitiwa mbaroni na kundi hilo katika miji ya Kut na Haskeh Mineh
Achin na kisha kufanywa watumwa wa ngono. Ameongeza kuwa, wanawake wengi
walikamatwa katika mji wa Achin ambao ni makao makuu ya genge hilo
nchini Afghanistan.
Aidha ameelezea ongezeko la vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya
wanawake na kusema kuwa, kwa mujibu wa ripoti zilizotolewa hivi
karibuni, jumla ya kesi 35 zimeripotiwa katika mji wa Herat tangu
mwanzoni mwa mwaka huu pekee. Mkuu wa Taasisi ya 'Uadilifu kwa ajili ya
Wote' nchini Afghanistan amesema kuwa siku chache zilizopita, mwanamke
mmoja alimwagiwa tindikali katika eneo la Bagh Bala mjini Kabul, huku
wanawake wengine wawili wakichomwa moto katika mkoa wa Nangarhar.
Kwa mujibu wa Hamideh Wardak, mwanamke mmoja ameripotiwa kufariki
dunia kwa kuchapwa bakora katika mkoa wa Urozgan kwa tuhuma za kukimbia
kuolewa na wanachama wa kundi hilo, na kwamba hayo ni matukio machache
sana yanayowakabili wanawake wa Afghanistan kipindi hiki. Kadhalika
amesema kuwa siku chache zilizopita wanawake wawili walishikwa na
wanachama wa kundi la Taleban katika mji wa Day Mirdad mkoa wa Maidan
Wardak, na kwamba wanachama hao wanataka kuwaoza kwa nguvu kwa kile
kinachoitwa Jihadun-Nikaah.
Kwa ajili hiyo Hamideh Wardak ameitaka serikali ya Afghanistan kuzuia
mwendelezo wa jinai za makundi hayo ya kigaidi dhidi ya wanawake na
kwamba kuendelea kimya cha serikali ni sawa na kufungua njia ya
mwendelezo wa ukatili na jinai hizo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: