UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE ZANZIBAR; MGOMBEA WA UPINZAMI ADAI NI 'VURUGU TUPU'
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:12 AM
Uchaguzi mdogo wa jimbo la ubunge la Dimani
viswani Zanzibar nchini Tanzania umefanyika leo huku chama kikuu cha
upinzani visiwani humo cha Wananchi (CUF) kikilalamikia kile kilichodai
kuwa ni ukiukaji mkubwa wa sheria na taratibu za uchaguzi.
Uchaguzi
huo umefanyika kujaza nafasi iliyoachwa wazi na mbunge wa jimbo hilo
kwa tiketi ya chama tawala cha Mapinduzi (CCM) Hafidh Ali Tahir
aliyefariki dunia mwezi Novemba mwaka uliopita wa 2016 ulitazamiwa
kushuhudia mchuano mkali baina ya mgombea wa chama hicho na yule wa CUF
anayewakilisha muungano wa upinzani wa UKAWA.
Hata
hivyo mapema leo Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa CUF Salim
Bimani alivieleza vyombo vya habari kuwa daftari la wapiga kura
lililotumika katika uchaguzi wa leo silo lililotumiwa katika uchaguzi
mkuu wa Oktoba 2015 na kwamba wapiga kura hewa wengi wamepiga kura
katika uchaguzi huo kwa maslahi ya CCM.
Wakati
huohuo mgombea wa ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CUF Abdulrazak
Khatib Ramadhani amemwandikia barua rasmi Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume
ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) kulalamikia kile alichodai uchaguzi wa
vurugu uliofanyika leo.
Taarifa
ambazo zimethibitishwa na mwandishi wa Radio Tehran zinaeleza kuwa
mawakala kadhaa wa vyama vya upinzani pamoja na waandishi wa habari
walitimuliwa kwenye vituo vya kupigia kura na askari wa jeshi la polisi
kwa tuhuma mbalimbali.
Hadi tunaelekea mitamboni matokeo rasmi ya uchaguzi huo yalikuwa bado hayajatangazwa…/
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: