TEMBELEA UKURASA MPYA WA UJIJIRAHAA WA KIMATAIFA: MWAKA MPYA WA 2017 NACHANGAMOTO ZINAZOUKABILI ULIMWENGU

Mwaka mpya wa 2017 umeanza leo sambamba na shambulizi lililofanyika katika klabalu moja ya starehe mjini Istanbul huko Uturuki na kuua watu karibu 40 na kujeruhiwa makumi ya wengine.
Tukio hilo ni ishara kwamba mwaka mpya wa 2017 huwenda ukatawaliwa na machafuko na umwagaji damu zaidi ya miaka iliyopita.
Ugaidi ambao katika miaka hii ya sasa umekuwa zimwi kubwa linalovuruga usingizi na usalama wa walimwengu kutokana na kupuuzwa vyanzo na sababu zake halisi na vilevile kutumiwa vibaya na baadhi ya nchi kwa malengo ya kisiasa, sasa umepanua mbawa zake katika maeneo mbalimbali ya dunia. Inaonekana zimwi hilo la ugaidi litatafuna idadi kubwa zaidi ya wanadamu katika mwaka huu wa 2017 na kuenea katika maeneo mengine ya dunia. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, kushindwa mtawalia kundi la Daesh na magaidi wengine katika nchi za Syria na Iraq kumewafanya wanachama wa makundi hayo warejee katika nchi zao huko Ulaya, Marekani na kaskazini mwa Afrika, suala ambalo ni hatari kubwa kwa maisha ya watu, usalama na amani ya nchi hizo.

0 comments: