SHEKHE WA WILAYA YA KIGOMA AWAASA WAISLAMU KIGOMA

NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA

WAUMINI wa dini ya kiislam mkoani Kigoma wameaswa wasitumie kitabu cha dini(QUR`AN)  kuleta mifarakano katika jamii ili,kutimiza utashi wenye maslai ya kuigawa dini hiyo katika makundimakundi,badala yake waijenge  dini kwa mshikamano wenye tija kwa umati wa Mtume Muhamad( SWA).


Akitoa kauli hiyo mbele ya umati wa waumini hao hivikaribuni Kigoma Ujiji mkoani humo,kwenye madhimisho ya sherehe za Kuzaliwa kwa Mtume huyo,Shekhe Mkuu wa wilaya Kigoma,Alhaji Twalha Kiburwa alisema maadhimisho hayo yameratibiwa na  Jumuia ya Shia Ithnaasheri.

Alieleza kuwa,siku za hivi  karibuni  kuna baadhi ya waislam wamejiingiza katika  migongano ya wenyewe kwa wenyewe  inayochangia  ubaguzi baina yao,ambapo wanaofanya hivyo wanafanya kwa maslahi  binafsi  kwa kutumia aya na hadithi kadhaa katika vitabu vya dini kwa kujenga fitina zao.

Alifafanua kuwa,tofauti ya madhehebu miongoni mwa waislam siyo kigezo cha dhehebu moja kujiona  ni bora zaidi ya dhehebu linguine,kilichopo ni kuzingatia misingi ya Uislamu na si  tofauti za madhehebu kwa kuwa  hazina tija katika misingi ya kuwafanya wasiungane katika kuiendeleza dini.


Naye Mwenyekiti wa Bara la Afrika wa Taasisi ya Bilal Muslim, Muslim Abdallah Sheni amewakumbusha waumini wa dini hiyo wazingatie misingi ya dini inayowajenga kuwa na  upendo, amani na mshikamano ,badala ya kila mtu kufanya maelekezo ya dhehebu lake kuwa ndiyo msingi mkuu wa dini hiyo.

Sheni alisema  hawana budi kushirikiana katika kuitumikia jamii ikiwemo  kupeleka miradi mbalimbali ya kijamii  hasa huduma ya Afya,maji na nyinginezo, kwa kutumia taasisi zao,ili kuimarisha mahaba kwa dini hiyo ,kwa kila mwanajamii.
 Kwa upande wa Mwenyekiti wa Taasisi ya Bilal Muslim Mission mkoani Kigoma,Sheikh Abdulwahid Abayat alisema ili kurudisha umoja miongoni mwao hawana budi kuwajengea watoto  misingi ya dini kwa kuwafundisha matendo mema kwa kuwa wakarimu,wenye upendo na kumpenda kila mtu.

Shekhe Abayat alisema changamoto ya kufarakanamiongoni mwa dini hiyo,inachangiwa na kutoandaliwa vyema katika misingi stahiki ya imani  juu  watoto wa kiislam ikiwemo  maisha ya  kumcha mungu  ambapo ni silaha kwa jamii kuishi kwa amani na upendo

0 comments: