OBAMA AAGA, ASEMA UBAGUZI DHIDI YA WAISLAMU NCHINI MAREKANI HAUKUBALIKI

Rais Barack Obama wa Marekani ametahadharisha kuhusu mwenendo wa kudumishwa mifarakano na ubaguzi katika nchi hiyo.
Obama ambaye alikuwa akitoa hotuba ya kuaga Wamarekani katika mji wa Chicago baada ya kuiongoza Marekani kwa mihula miwili, amesema kuwa ubaguzi bado ni nguvu inayozusha mifarakano katika jamii ya Marekani. Vilevile ametahadharisha kuhusu hali ya kisiasa ya nchi hiyo na kusema: Ubaguzi wa kizazi ndio tishio kubwa kwa demokrasia ya Marekani.
Rais Barack Obama amesema ubaguzi unaofanywa dhidi ya Waislamu nchini Marekani haukubaliki.
Waislamu wa Marekani wanabaguliwa
Katika hotuba yake ya kuwaanga Wamarekani, Obama amesema kuwa makubaliano ya nyuklia ya kundi la 5+1 na Iran na kuanzisha tena uhusiano na Cuba ndiyo matunda muhimu zaidi ya kipindi cha utawala wake.
hata hivyo ongezeko la mauaji ya Wamarekani wenye asili ya Afrika na ukatili wa polisi ya Marekani wa kuwapiga risasi watu weusi ni tishio kubwa kwa jamii ya Marekani na mambo hayo yanailekeza kuzimu taratibu jamii ya nchi hiyo.
Ripoti zinasema kuwa, Mmarekani mmoja mwenye asili ya Afrika huuliwa kwa kupigwa risasi na polisi kila baada ya masaa 28 nchini Marekani, na hicho ndicho kiwango cha juu zaidi cha kuuliwa watu weusi duniani.
Wamarekani wakiandamana kupinga mauaji yanayofanywa na polisi dhidi ya Wamarekani weusi
Kipindi cha uongozi wa miaka 8 ya Barack Obama kinamalizika wiki ijayo kwa kuapishwa rais mteule wa Marekani Donald Trump.

0 comments: