MKUU WA JESHI LA POLISI NCHINI, IGP ERNEST MANGU ATUMA TIMU YA MAOFISA WA JESHI LA POLISI KWENDA ZANZIBAR KUCHUNGUZA VITENDO VYA UDHALILISHAJI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 5:05 AM
Mkuu wa
Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu ametuma timu ya Maofisa wa
Polisi ikiongozwa na Kamishna wa Polisi Jamii Mussa Alli Mussa kwenda
Zanzibar kushughulikia kero na malalamiko ya wananchi juu ya vitendo vya
udhalilishaji na ukatili kwa watoto/wanawake ambavyo vimekuwa
vikiripotiwa mara kwa mara.Timu hiyo imepewa jukumu la kuchunguza
vitendo hivyo vya udhalilishaji na kiini chake na hatimaye kuja na
mpango mkakati wa kuzuia vitendo hivyo ikiwemo kuwakamata wahusika na
kuwafikisha mahakamani.
IGP Mangu
amewataka wananchi wa Zanzibar, Taasisi za kiserikali na Taasisi za
kiraia zilizopo Zanzibar kutoa ushirikiano kwa timu hiyo ili kukomesha
vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na maadili ya Watanzania.
Imetolewa na:
Advera John Bulimba - ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Polisi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: