MIAKA 53 YA MAPINDUZI “WAZO LA DKT MOHAMMED SEIF KHATIB KUANZISHA MAKUMBUSHO YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR LIFANYIWE KAZI”
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 2:23 PM
Na
Judith
Mhina – MAELEZO
“Wakati umefika wa
kujenga makumbusho ya Taifa ya Mapinduzi
ya Zanzibar, ili kizazi cha sasa na kijacho waweze kujifunza na kuipitia
historia muhimu kwa Watanzania na wageni kutoka nje.
Hayo ni maneno ya
msingi ambayo yamesemwa na Dkt Mohammed Seif Khatibu wakati wa mahojianno yake
na Idara ya Habari MAELEZO mapema mwishoni mwa wiki.
Dkt Khatib
alisisitiza “Ni vema kuonesha katika picha, maandishi na sura halisi za historia
ya Zanzibar kabla yaani wakati wa Waajemi, Wareno, Waarabu, Waingereza na sasa
Serikali ya Mapinduzi”.
Dhamira ya makumbusho
hayo, Dkt. Khatib amesema “Vijana wengi ukiwaambia nchi hii kulikuwa na
unyanyasaji wa Waafrika hawakubali maana hawajui historia, waelezwe kwa nini
tuko huru, kuna wasioitakia mema Zanzibar wanapotosha historia hiyo”.
Kumbe kwa kuweka
makumbusho na usahihi wa historia ya nyuma kabla, wakati, baada ya Mapinduzi na
yanayotokea sasa, hayo yote yakiwa katika makumbusho yatakuwa msingi wa
historia ya Zanzibar hatua ambayo itasaidia kuwekwa wazi mambo yaliyowahi
kutokea, hivyo sio rahisi kwa mtu yoyote ambaye ana agenda ya kupotosha umma
kufanya hivyo.
Lakini kwa sasa ni
kweli kabisa mtu yoyote anaweza akasema vyovyote atakavyo kwa kuwa hawajui historia
na wala hawana mahali pa kurejea historia ya Mapinduzi ya Zanzibar.
“Watu walitoka Kongo,
Malawi, Kigoma na Tabora wakibebeshwa pembe za Ndovu na kusafiri kwa mguu, wakifuata njia ya reli ya kati, mpaka
Bagamoyo na kusafirishwa na boti mpaka Unguja
na kuwekwa sokoni kuuzwa kama samaki katika soko la watumwa. Huu ndio ukweli”
alisema Dkt Khatib.
Tuchukulie mfano wa
jirani zetu Rwanda walikubwa na mauaji yakimbari mwaka 1994, kwa kutambua kuwa
hicho siyo kitu kizuri kutokea tena hapa duniani wameona waweke makumbusho ya
kitaifa. Inahuzunisha lakini ndio ukweli, unapoona yale mafuvu ya vichwa
yalivyopangwa huwezi kuamini kama hiyo ni hali halisi iliyotokea hapa duniani.
Kwa Wanyarwanda na
watu wengine duniani, makumbusho kimbari ni sehemu ya Utalii ikizingatia msemo
wa waswahili wanasema kuona ni kuamini.
Siyo hiyo, tu hata
kule Namibia kuna jumba la makumbusho la mauaji yaliyofanywa na wajerumani kwa
kabila la Waherero waliuwawa katika vita ya kwanza ya dunia. Takribani Waherero
nusu ya milioni waliuwawa na hivi karibuni Waherero wa Namibia walikuwa
wanaomba fidia kwa Serikali ya Ujerumani, ingawa Ujerumani wameomba msamaha kwa
mauaji hayo ya kimbari.
Uingereza ni nchi inayoongoza
duniani kwa kuweka kumbukumbu zake katika makumbusho za Kifalme, Kimataifa,
Kitaifa, Vita, Silaha, Bahari, Mtu Binafsi, Jiji au Mji husika. Uingereza ina
zaidi ya makumbusho 55 ambayo yanafahamika duniani. Mfano “British Museum London, Natural History Museum
London, National Gallery London, Science Museum London, Victoria and Albert Museum,
National Maritime Museum, Museum of London City, National Portrait Gallery,
National Army Museum, Sir Johns Soanes
Museum, Wallace Collection London, National War Museum nk”
Hivyo, tuunge mkono
wazo hilo na tushirikiane wote kama Watanzania kuhakikisha kituo hicho cha
makumbusho kinajengwa na kuhifadhi kila kinachohitajika ili kukamilisha
historia husika.
Kujengwa kwa kituo
cha makumbusho Zanzibar kitasaidia kuingizia fedha kama sehemu ya Utalii wa
historia ambapo mtu anayehitaji kuijua historia hiyo atapata kila kitu mahala
pamoja bila kusumbuka. Mungu ibariki
Tanzania “MAPINDUZI DAIMA”.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: