Mkurugenzi
Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan
Abbasi akizungumza na waandishi wa habari hawapo (pichani) kuhusu
kukamatwa kwa mmiliki wa Kampuniya FAKUNA ambaye anatuhumiwa kutaka
kuitapeli Serikali baada ya kubainika kuwasilisha nyaraka za kughushi
ili asajili Gazeti la Lete Mambo leo jijini Dar es Salaam.Kulia ni Kaimu
Msajili wa Magazeti Patrick Kipangula na kushoto ni Afisa Habari wa
Idara ya Habari MAELEZO LilianLundo.
Baadhi ya
waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Habari –
MAELEZO alipokuwa akitoa taarifa juu ya kukamatwa kwa mtuhuhiwa
aliyejaribu kughushi nyaraka za Serikali ili asajili Gazeti leo jijini
Dar es Salaam.
Mtuhumiwa
wa kughushi nyaraka za Serikali ili asajili Gazeti ambaye pia ni
mmiliki wa Kampuni ya FAKUNA Bw. Joseph Sheka akitolewa ndani ya Ofisi
za Idara ya Habari – MAELEZO punde baada ya Mkurugenzi wa Idara ya
Habari – MAELEZO kumkabidhi mtuhumiwa huyo mikononi mwa jeshi la Polisi
kwa ajili ya hatua zaidi.
Pichani
mtuhumiwa Joseph Sheka akiongozwa na Askari Kanzu kuelekea kwenye gari
la Polisi tayari kwa kupelekwa Kituo cha Polisi Kati leo jijini Dar es
Salaam.Sheka anatuhumiwa kutaka kuitapeli Serikali kwa kuwasili shanyara
kazakughushi katika Ofisi za Msajiwa Magazeti ilia pate usajili wa
Gazeti la Lete Mambo.
Watuhumiwa
wakiwa ndani ya Gari la Polisi mara baada ya kukamatwa na kukabidhiwa
kwa jeshi la Polisi leo jijini Dar es Salaam. Watuhumiwa hao
wamefikishwa katika Kituo cha Polisi cha Kati kwa mahojiano zaidi na
hatua zingine zitafuatia.
Pichana: Frank Shija – MAELEZO.
Na Jacquiline Mrisho.
Idara ya
Habari (MAELEZO) imebaini nyaraka za kughushi zilizowasilishwa na
Mmiliki wa Kampuni ya FUKANI, Joseph Sheka wakati alipoziwasilisha kwa
ajili ya kusajili gazeti la LETE MAMBO.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa MAELEZO,
Dkt. Hassan Abbasi amesema kuwa mtuhumiwa huyo aliwasilisha nyaraka
mbalimbali akidai kuwa ni za Mamlaka ya Mapato (TRA) ambazo uchunguzi wa
awali umebaini kuwa mihuri na sahihi za baadhi ya maafisa wa Mamlaka
hiyo zilizotumiwa ni za kughushi.
“Ni vyema
jamii ikafahamu kuwa huu sio wakati wa kujaribu kuishi kwa njia zisizo
halali, kila mwananchi anapaswa kufuata taratibu zinatohitajika pindi
anapotaka kupatiwa huduma katika maeneo mbalimbali ya ofisi za Umma.
Dkt.
Abbasi alitoa rai kwa ofisi mbalimbali za Umma kuwa makini na nyaraka
zinazowasilishwa na wateja wao kwani zinaweza kuwa na malengo mbalimbali
ya kuiingiza Serikali katika matatizo hivyo kuitia hasara.
Mbali na
hayo Dkt abbasi alisisitiza kuwa wale wanaohisi waliwasilisha nyaraka
zao na kuona kwamba zina utata kuja kuzirekebisha na watakaobainika kuwa
walighushi nyaraka hizo sheria itafuata mkondo wake.
Kwa sasa Idara ya Habari imemkabidhi mtuhumiwa katika Kituo cha Polisi cha Kati jijini dar es salaam kwa mahojiano zaidi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: