ALIYEKUWA WAZIRI MKUU ATEULIWA KUWA MAKAMU WA RAIS WA IVORY COAST
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:25 PM
Rais Alassane Ouattara wa Ivory Coast
amemteua aliyekuwa Waziri Mkuu Daniel Kablan Duncan kuwa Makamu wa Rais,
cheo kipya ambacho kimeundwa kupitia katiba mpya ya nchi hiyo
iliyopitishwa kwa Kura ya Maoni iliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana.
Duncan,
mwenye umri wa miaka 73 ambaye kitaaluma ni mchumi, amehudumu katika
Benki Kuu na pia kama Waziri wa Fedha katika nchi hiyo ya magharibi mwa
Afrika na ni miongoni mwa washirika wa karibu na wa muda mrefu wa Rais
Ouattara. Alijiuzulu wadhifa wake wa uwaziri mkuu hapo jana na kuvunja
serikali ili kupisha mchakato wa utekelezaji katiba mpya.
Akihutubia
bunge wakati wa kumtambulisha makamu wake, Rais wa Ivory Coast amesema
Duncan ni mtu mwenye uzoefu, mtumishi mkubwa kwa serikali na ambaye
ameonyesha sifa za kipekee za kishakhsia na kitaalamu alizonazo katika
nyadhifa zote za juu alizowahi kushika.
Cheo cha Umakamu wa Rais kiliingizwa katika katiba mpya ya Ivory
Coast iliyopitishwa mwezi Novemba mwaka jana ili kuhakikisha upokezanaji
wa madaraka unafanyika kwa amani itokeapo rais kufariki dunia au
kupoteza uwezo wa kutekeleza majukumu yake wakati akiwa angali
madarakani.
Wakodiva
wengi pia wanaiona hatua hiyo kama wenzo wa kumwezesha rais Alassane
Ouattara kuandaa mrithi wake wakati kipindi chake cha uongozi
kitakapomalizika mwaka 2020…/
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: