Haki miliki ya picha DAVID CRIGGER/BHCImage captionNick Stafford alikodisha toroli tano kusafirisha malipo ya kodi yake.
Mfanyibiashara
mmoja nchini Marekani ambaye amezozana na idara ya magari nchini humo
DMV amelipa kodi yake ya dola 3,000 kwa kutuma mikokoteni mitano iliojaa
sarafu 300,000
Nick
Stafford kutoka Cedar Buff, Virginia, aliwasilisha sarafu nyingi hatua
iliolazimu mashine ya kuhesabu sarafu hiyo ya Idara hiyo kushindwa
kuzihesabu.Hatua hiyo inajiri kufuatia mgogoro kati yake kuhusu
kuwasiliana na wafanyikazi kuwauliza kuhusu kodi yao.Iliwalazimu
wafanyikazi kutumia saa saba wakihesabu sarafu hizo hadi usiku.
Walimaliza kazi hiyo ya kuhesabu mapema siku ya Alhamisi.Haki miliki ya pichaDAVID CRIGGER/BHCImage captionBwana Salford alikuwa na sarafu 300,000
Bwana
Stafford aliambia BBC aliwasilisha pingamizi yake kwa sababu alizitaka
idara za serikali kuangazia na kutoa majibu kwa maswala yanayowakumba
raia."Haijalishi iwapo utalipa dola 300 kwa mwaka kama kodi au dola 3000
kwa mwaka kama mimi kwa sababu uti wa mgongo wa taifa lililo na
demokraisa huru ni sharti liwe na serikali ilio na uwazi, alisema.Bwana
Stafford ameelezea katika mtnadao wake kwamba mgogoro wake na DMV
ulizuka kwa sababu idara hiyo haikutaka kumpatia nambari za simu za moja
kwa moja kuhusu afisa wa kuwasiliana naye ili kusajili magari matatu na
kulipa ushuru kwa kuwa anamiliki nyumba tatu katika maeneo 3 tofauti.
Aliwasilisha
ombi la kutaka kupewa nambari ya moja kwa moja kulingana na Bristol
Herald Courier na akapewa nambari ya simu ambayo angepiga.Lakini
alipoitumia aliambiwa kwamba haingeweza kuitumia kuuliza maswali.Bwana
Stafford alitaka kujua nambari hizo za moja kwa moja za maafisa wengine
tisa ijapokuwa Idara hiyo tayari ilikuwa imemshughulikia swala lake.
Na ombi lake lilipokataliwa alienda mahakamani kuwasilisha malalamishi yake.
Mapema
wiki hii jaji mmoja alipinga maombi yake matatu aliowasilisha ,akikataa
maombi alilowasilisha kwa DMV na wafanyikazi wake wapigwe faini.
Hatahivyo
wafanyikazi wa idara ya magari baadaye walimpatia nambari hizo
alizotaka na tayari amezichapisha katika mtandao wake.Bwana Stafford
anasema kuwa idara ya magari ililazimika kukubali malipo yake kwa sababu
sheria ya Marekani kuhusu sarafu mwaka 1965 inasema sarafu ni fedha
halali na zinaweza kutumika kulipa madeni, kodi na mishaharaHaki miliki ya pichaDAVID CRIGGER/BHCImage captionIdara ya ushru nchini Marekani ilitumia wakati mwingi kuhesabu fedha hizo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: