WAPINZANI WAPAMBANA NA POLISI JAMHURI YA KKIDEMOKRASIA YA KONGO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:14 PM
Maandamano ya nchi nzima huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) yamewalazimisha polisi kuingilia kati kukabiliana nayo.
Mtandao wa habari wa Africa News
umeripoti habari hiyo leo na kusema kuwa, maandamano hayo yamefanyika
leo kulalamikia kufungwa jela wanaharakati 15 wa kisiasa wanaoipinga
serikali ya Rais Joseph Kabila. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mahakama moja
ya DRC imewahuku kifungo cha miaka mitatu jela wanaharakati 15 wa
kisiasa wa nchi hiyo kwa tuhuma za kufanya uasi na kuvuruga utulivu na
usalama wa umma.
Ijapokuwa vyombo vya mahakama vya Kongo
vimewaachilia huru wanaharakati 34 wa kisiasa kama njia ya kutuliza hali
ya mambo, lakini machafuko yameongezeka kutokana na kuendelea kubakia
madarakani Rais Joseph Kabila licha ya muda wake wa urais kumalizika
tarehe 19 mwezi huu wa Disemba.
Duru za kuaminika zimesema kuwa, idadi ya waandamanaji waliouawa
kwenye maandamano ya kupinga serikali inazidi kuongezeka na hivi sasa
imeshapindukia watu 30. Ikumbukwe kuwa serikali ya Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo imepiga marufu maandamano nchi nzima.
Wakati huo baadhi ya duru za DRC
zimetangaza kuwa, jana usiku mazungumzo baina ya serikali na wapinzani
yalianza kwa upatanishi wa viongozi wa kidini wa nchi hiyo.
Rais Joseph Kabila, aliyeingia
madarakani baada ya kuuliwa baba yake, Laurent Desire Kabila mwaka 2001
ameshashiriki kwenye chaguzi mbili za mwaka 2006 na 2011 na kushinda.
Kwa mujibu wa Katiba ya Kongo, Joseph Kabila hana haki ya kushiriki
kwenye uchaguzi mwingine baada ya kuwa Rais kwa vipindi viwili
mfululizo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: