WAISLAMU ELFU 50 WA MYANMARI WAMEKIMBILIA NCHINI BANGLADESH
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 9:23 PM
Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Bangladesh
imetangaza kuwa, Waislamu elfu 50 wa jamii ya Rohingya huko nchini
Myanmar wakimbilia katika nchi hiyo hadi sasa kujinusuru na vitendo vya
ukandamizaji dhidi yao.
Taarifa ya Wizara ya Mashauri ya
Kigeni ya Bangladesh imeeleza kuwa, raia takribani elfu 50 wa jamii ya
Waislamu wa jimbo la Rakhine kutoka katika jamii ya wachache ya Rohingya
wamekimbilia nchini humo kujiokoa na vitendo vya ukandamizaji na
utumiaji mabavu dhidi yao vinavyofanywa na mabudha wa Myanmar.
Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya
Banglaesh imemuita balozi wa Myanmar mjini Dhaka na kumuelezea wasiwasi
iliyonao nchi hiyo kutokana na kuendelea vitendo vya ukandamizaji na
utumiaji mabavu dhidi ya Waislamu wa jamii ya wachache ya Rohingya
nchini Mynamar.
Wakati huo huo, serikali ya Bangladesh
imewataka raia laki tatu wa Myanmar wanaoishi kinyume cha sheria nchini
humo kurejea makwao.
Ripoti mbalimbali zinaeleza kuwa, jumuiya za misaada ya kibinadamu
pia haziwasaidii Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar ambao
wanazingirwa na jeshi la nchi hiyo.
Katika miaka ya karibuni, Waislamu wengi
wa kabila la Rohingya nchini Myamnar wameuawa au kulazimika kuhama
makazi yao na kuwa wakimbizi katika nchi za Thailand, Malaysia na
Indonesia kutokana na mashambulio ya Mabudha wenye misimamo ya kufurutu
mpaka wanaoungwa mkono na serikali ya nchi hiyo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: