SIMULIZI ZA KUSISIMUA : SIKU ANDY CHANDE ALIPOITWA IKULU YA JULIUS NYERERE...
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:40 PM
Ikafika siku hiyo Andy akaitwa na
rafiki yake Julius aende Ikulu. Hata alipoingia Ikulu, Andy alimwona
Julius mwingine. Hakuwa mcheshi kama ilivyokuwa kawaida yake. Julius
akamwambia Andy akae kitako na hapo hapo akamfahamisha maamuzi ya
kutaifisha kiwanda chao na kuwa Shirika la Umma.
Na cha ajabu, Julius akamwomba rafiki yake Andy awe Mwenyekiti wa Kwanza wa Bodi ya National Milling Cooperation!
Andy akakubali! Na akaifanya kazi ile kwa nguvu zake zote.
Inasikitisha kuona leo Andy anaanikwa
kwenye magazeti ya udaku na kutolewa taswira hasi. Tena ni Andy huyu
huyu ambaye aliwahi kuwa mmoja wa wajumbe wa Tume iliyokuwa ikipitia
filamu zote zinazoingizwa Tanzania kuziangalia kabla umma haujaonyeshwa.
Lengo lilikuwa kuhakikisha kuwa filamu hizo za kigeni haziathiri
maadili, mila na utamaduni wetu.
Leo Andy amekuwa mhanga wa baadhi ya
vyombo vya habari vinavyokiuka maadili, mila na utamaduni wetu, kwa
kumuanika hadharani, tena kwa kuweka picha zake, bila ridhaa yake, kuwa
ni mwanachama wa jumuiya ya Freemasons, jumuiya ambayo, kwa kupotosha
umma, media inadai wanachama wake wanaamudu mashetani!
Andy Chande hajawahi kukana kuwa
mwanachama wa Freemasons. Hilo pia ameliandika kwenye kitabu chake. Ni
wengi wasiojua Freemasons ni nini. Nitaliandika hili la Freemasons, na
hata Andy mwenyewe anavyolielezea.
Naam, kuna waliamua kutetea uvivu wao kwa kusingizia Freemasons!
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: