MWAKA MMJA WA GOBIG NA MAFANIKIO MAKUBWA NA HAKUNA NDOTO KUBWA DUNIANI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:56 AM
Na: Meshack Maganga- Mwanzilishi wa GoBigDevelopment Network-Tanzania.
Kwenye
Jamii Yetu Imezoeleka kwamba, Mfanikio kwenye maisha yapo ofisni ama
kwa kuwa na cheo kikubwa . Katika makala hii fupi, nitaelezea kwa kifupi
historia ya GoBigDevelopment Network, kikundi kilichoanza kwenye
mtandao wa kijamii na kuwa kundi lenye mvuto na mafanikio makubwa sana
kwa wanachama wake.
Nilipoandika makala niliyoipa kichwa cha “Waliofanikiwa Hawaishi Kwenye Sayari Ya Proxima Centauri”
Nililezea kwa kifupi jinsi ya kujiamini na kutumia mazingira yetu ya
hapa hapa Tanzania ili kufikia malengo na ndoto zetu (Sisi wote
tumesikia kauli Mbiu ya Serikali yetu HAPA NI KAZI TU). Nilieleza jinsi
ambavyo watanzania na hasa vijana wanavyoweza kutumia fursa zilizopo
kujiondoa kwenye umasikini wa kujitakia na pia kuacha tabia ya
kulalamika sana bila kuchukua hatua.
Katika
makala ile, nilipata mwitikio mkubwa sana. Kwanza, nilipigiwa simu
nyingi na kutumiwa barua pepe nyingi, baadhi ya wasomaji walikuja
‘chemba’ kwa lugha ya mkoloni wanaita in box katika mazingira ya
mitandao ya kijamii . Wengi wakipongeza na kuomba kujiunga na GoBig
Development Network.
Historia
Ya “GoBig Development Network” inaanzia mbali sana miaka saba iliyopita
nilipoanza kusoma vitabu vingi na kukutana kitu kinaitwa “The Power of
the Master Mind”, nikaanza kujiunga na makundi mbalimbali kwenye jamii
na marafiki zangu wale wenye malengo makubwa na wale ambao wanaona
uthamani wa wao kuwepo Dunini, kuwepo Afrika,na zaidi kuwepo ndani ya
nchi tukufu,nchi hii kubwa ya ajabu na yenye fursa nyingi za kiuchumi
iitwayo Tanzania.
Baada
ya kuibuka kwa mitandao mingi ya kijamii ikiwemo “FaceBook, WhatSSAP,Na
mingine mingi zikiwemo blogs nikakutana na marafiki wengi sana
wanaowaza kama mimi, mwenye kiu ya mafanikio.nikajiunga na makundi hayo.
Moja ya makundi ninayokumbuka mpaka sasa ni kundi liitwalo “Wakulima wa
kisasa” lilinzishwa Dada Fulani mkulima wa Embe na mihogo. Lilinisaidia
sana.
Kimsingi,
GoBig Development Network imekuja kuanza rasmi miaka miwili iliyopita,
kwenye ukurasa wangu wa face book, nilikuwa nikiandika ama kuweka
picha, kila mwisho wa posti yangu nilikuwa nikiandika Maneno haya ‘GoBig
Or Go Home and Watch Tv’. Nikiwa na maana kwamba, binadamu wote tuna
uwezo sawa tuliopewa na Mungu na sasa una kuwa na chaguzi mbili, ukiona
fursa, ni wajibu wako kuifanyia kazi ili ufanikiwe ama uendelee kukaa
nyumbani kwako ukiangalia Tv.
Mwaka
2015, nikafungua grupu la whatssap liitwalo “GoBig Or Go Home” nilianza
kwa kuwakaribisha marafiki zangu wachache, tulianza kupeana fursa
mbalimbali za hasa kilimo . Tulianza kufundishana fursa za kilimo
biashara kama ,kilimo cha matunda, ufugaji wa Ng’ombe, mbuzi, bata
mzinga,kuku, ufugaji wa nyuki,kilimo cha miti nk. Mwitikio ulikuwa
mkubwa sana, kutoka wanachama 8, ambao nilianza nao siku ya jumamosi
tarehe 18.12.2015 mpaka kufikia wanachama 67 ilipofika mwezi wa kwanza
mwaka huu unaoisha wa 2016.(P.T)
Limekuwa
ni Grupu la mfano wa kuigwa, watu wamehamsika sana. Mkazo uliwekwa
kwamba kila mtu anae jiunga GoBig, lazima awe na kitu ana fanya huko
kwake, yaani awe analima, hata kama ni kwa nusu ekari, awe anafuga hata
kama ni kuku watano, ama awe anafuga samaki, nyuki, ana panda miti nk.
Nilianza
kutafuta watu wenye mafanikio makubwa kwenye kilimo, na ufugaji na
kuwaomba Muda wao, waje kwenye Grupu la GoBig, ili waweze kutoa hamasa,
walikubali bila malipo na kutumia muda wao kuja kutufundisha kilimo hii
ikawa mwanzo wa mafanikio makuba sana tuliyoyapata kama kikundi.
Nimekuja
kuamini kwamba, hapa duniani HAKUNA NDOTO KUBWA YA KUMSHINDA MWANADAMU
ANAEPAMBANA . Nimeamaini tena kwamba maisha yenye mafanikio ni vitendo
na si ndoto pekee, ndoto ni mwanzo tu wa maisha. Maisha ni kuchukua
hatua na si kufikiri pekee. Maisha ya kijasiriamali ni kusonga mbele na
si kupiga kele za lawama peke yake. Katika yote uliyochagua maishani
kuwa mtendaji, usikubali kuyaishi maneno ishi matendo.
Kuanzia
mwezi wa pili mwaka 2016, tulianza kufanya ziara mbalimbali za
kuwatembelea watu wenye mafanikio kwenye mikoa ya Tanzania bara. Kwanza
tulianza na mkoa wa Iringa, tulitembelea vituo vya kilimo kama Baltony,
kujifunza kilimo cha umwagiliaji, tuliwatembelea wakulima wa miti,
wakulima wa vitunguu na Nyanya na kuweka mkazo kwa kila mwanachama wa
GoBig kuanza mchakato wa kufanya uwekezaji kwa kitu anachokipenda.
Mwitikio umekuwa mkubwa sana.
Aidha,
tulisafiri kwa nyakati tofauti na kwenda mkoa wa Mbeya hasa wilaya ya
Rungwe na kukutana na wakulima wakubwa wa Parachichi, Chai, Ndizi,
nyanya na ufugaji wa ng’ombe wa maziwa kisasa. Mikoa mingine ambayo
tumefika kama kikundi cha wajasiramali ni Mkoa wa pwani, Morogoro nk.
Kwakuwa
Asimilia kubwa ya vijana wakitanzania, wamekuwa wakilalamika sana
hasa kwa kukosa mitaji, sisi kwenye kikundi chetu cha GoBig, tumepiga
marufuku ulalamishi na akionekana mwanachama anaetoa visingizio vya
mitaji tunachofanya ni kumwambia aondoke haraka ili aingie mtaani
kulalamika zadi. Jambo la kujuliza ni hili, unalalamika huna mtaji
wakati sehemu kubwa ya aridhi yetu Tanzania haijatumika, unaweza kulima
matuta matano ya kabichi, ukawa unaingiza hadi laki mbili kila
unapovuna. Unaweza kulima mchicha, matuta kumi na baada ya siku kumi na
nne ukaanza kupata pesa na ukivumilia ukapata mtaji mkubwa kupitia huo
mchicha. Tunakosa mtazamo sahihi wa kipi tunakitaka. Kuna mapori makubwa
ndani ya hayo mapori unaweza kufuga nyuki kwa mtaji mdogo sana. Usiseme
hakuna pesa, Usisema pesa zimepotea, sema mimi nimepotea, sema sina
pesa, pesa zipo nyingi sana, fursa za kumwaga…Unachotakiwa kufanya ni
–KUGOBIG.
Miezi
mitano baadae yaani Tarehe 17.7.2016, GoBig Development Network
Tulipata bahati ya kumtembelea aliyekuwa waziri mkuu wa awamu iliyopita
,Mh. Pinda, hii ilikuwa ni bahati Ya kipekee sana kwetu. Tulijifunza
mambo mambo makubwa sana na hasa ya kubadilisha fikra, ninakumbuka swali
moja ambalo Mh. Waziri mkuu mstaafu, alituuliza sisi kama Wana-GoBig,
kwamba, “Wanangu hivi inakuwaje mtu ushindwe hata kupanda mashina kumi
ya papai?, unashindwaje kuwa na miembe mashina kumi ya miembe kijijini
kwenu ? Baada ya ziara hii iliyokuwa na mafanikio makubwa sana kwetu,
wengi wetu tulianza kufikiri tofauti.
Kwa
kuhitimisha Historia hii fupi ninaweza kusemakwamba kikundi cha GO BIG
DEVELOPMENT NETWORK ni fungamano huru la wajasiriamali wanaoshughulika
na shughuli za maendeleo katika nyanja za kilimo,ufugaji wa aina
mbalimbali,uwekezaji,na biashara. Na lengo letu kubwa ikiwa ni
kuhakikisha tunapiga vita umaskini na umaskini wa kifikra.
HAKUNA NDOTO KUBWA,
Chagua kufanikiwa,chagua Ku-Gobig, kijaze kichwa fikra za kufika sehemu
ambayo utaona kwamba, maisha yanawezekana. Badilili mtindo wako wa
kufikiri na taarifa zinazoingia ndani ya kichwa chako ziwe ni zile
zinazokupamoyo wa kufanikiwa. Ikumbukwe kwamba, mafanikio yanatokana na
mawazo au wazo la mafanikio. Wazo linatengeneza fursa na kama utabuni
wazo jipya kwenye mazingira yako utaibuka kuwa mshindi.
Fursa
za mafanikio zina gaharama yake, kuna gharama ya muda, gharama ya pesa,
na kama haupo tayari kulipia hizo gharama hizo fursa zitakupita.
Uchaguzi unabakia kuwa wako. Binadamu wote wenye mafanikio duniani
hawachoki kutafuta..! KARIBUNI SANA-GoBig
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: