KUSHAMIRI VITA YA MANENO BAINA YA DONALD TRUMP NA RAIS OBAMA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:18 PM
Sambamba na kukaribia siku ya kuapishwa rais
mpya wa Marekani yaani tarehe 20 ya mwezi ujao wa Januari kumeshadidi
vita vya maneno baina ya Donald Trump Rais mteule wa Marekani na Barack
Obama rais wa nchi hiyo anayemaliza muda wake wa uongozi.
Rais mteule Donald Trump
amemtuhumu Rais wa sasa wa Marekani Barack Obama kwamba, anatoa matamshi
ya uchochezi na kukwamisha mwenendo wa ukabidhianaji madaraka. Trump
ameandika katika ukurasa wake wa mtadano wa kijamii wa Twitter kwamba,
atafanya juhudi zake zote kuhakikisha kwamba, anayapuuza matamshi ya
uchochezi ya Obama pamoja na hatua za rais huyo za kukwamisha mambo.
Hivi karibuni Rais Obama alitangaza kwamba, ana uhakika kuwa kama Katiba
ya Marekani ingemruhusu agombee tena kiti cha uarsi kwa mara ya tatu
basi angeibuka na ushindi.
Zimebakia siku 21 tu kabla ya kumalizika kipindi cha uongozi wa miaka
8 cha Rais Obama ambapo Donald Trump ataapishwa na kuwa Ris wa 55 wa
Marekani. Katika kipindi hiki cha mpito ambacho kilianza siku moja baada
ya kufanyika uchaguzi wa Marekani Novemba 20 hadi atakapoapishwa rais
mpya, Obama amekuwa akifanya juhudi za kuimarisha mambo aliyoyaanzisha.
Hii ni katika hali ambayo, Rais mteule
Trump anafanya kila awezalo kuzuia kufikiwa lengo hilo la mtangulizi
wake. Kwa mfano katika hali ambayo, Rais Obama alikataa kutia saini
ujadidishaji wa vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran, Trump aliibuka na
kusema kwa mara nyingine kwamba, makubaliano ya nyuklia na Iran yana
madhara.
Fauka ya hayo, hatua ya kujizuia serikali ya Obama kupinga kura dhidi
ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Baraza la Usalama la Umoja wa
Mataifa nayo ilitajwa na Donald Trump kwamba, ni pigo kubwa kwa utawala
wa Kizayuni wa Israel. Aidha katika siku zake hizi za mwisho uongozini,
Obama ametia saini amri ambayo kwa mujibu wake uchimbaji mafuta katika
maeneo ya ncha za dunia utakuwa mgumu mno katika kipindi cha uongozi wa
Trump.
Donald Trump na washauri wake
wanaituhumu serikali ya Rais Obama kwamba, inakusudia kuchukua maamuzi
ambayo yatakwamisha utendaji wa serikali ijayo ya nchi hiyo chini ya
uongozi wa Trump. Hii ni katika hali ambayo, serikali ya Obama ina
wasiwasi wa kuondolewa urithi wake na mambo iliyoyaanzisha. Newt
Gingrich, mmoja wa waungaji mkono wakuu wa Trump alitangaza hivi
karibuni kwamba, katika serikali ijayo kwa akali asilimia 70 ya mambo
yaliyoachwa na serikali ya Obama yataondolewa na kufutiliwa mbali. Sera
za ulipaji kodi, uhajiri, afya, na bima nafuu ya matibabu inayojulikana
kama ObamaCare ni miongoni mwa mambo hayo.
Wakati huo huo, utanuaji misuli wa Trump
dhidi ya waitifaki wa Washington na vile vile hujuma yake ya maneno
dhidi ya Umoja wa Mataifa hususan baada ya kupasishwa azimio katika
Baraza la Usalama la umoja huo dhidi ya ujenzi wa vitongoji vya walowezi
wa Kiyahudi katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina ni mambo
ambayo kwa hakika yanaonyesha kuweko utendaji tofauti baina ya serikali
ijayo ya Trump na ile ya Obama inayomaliza muda wake.
Sambamba na tofauti hii kubwa ya mitazamo baina ya serikali ya sasa
na ijayo ya Marekani, hivi sasa walimwengu wanashuhudia kushadidi
mashambulio na vita ya maneno kati ya Obama na Trump huku zikiwa
zimebakia siku chache tu kabla ya tarehe 20 Januari siku ya
ukabidhianaji madaraka nchini humo.
Vita hivyo vya maneno vimeongezeka kiasi
kwamba, Julián Castro Waziri wa Nyumba na Ustawi wa Miji wa serikali ya
Obama amesema kuwa, Donald Trump ni mtu wa kushukiwa na mfisadi zaidi
ambaye amewahi kushinda uchaguzi wa Rais nchini Marekani hadi sasa.
Katika upande wa pili wa sarafu pia,
waungaji mkono wa Trump wanaamini kwamba, Obama ameipeleka Marekani
upande wa kudhoofika na kulegalega.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: