HABARI ZA KIMATAIFA, WATU 50 WAFA KWA MAFURIKO KATIKA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 8:34 PM
Kwa uchache watu 50 wamepoteza maisha, makumi
kadhaa wamejeruhiwa na maelfu ya wengine wamebaki bila makazi kutokana
na mafuriko yaliyotokea katika mji wa bandari wa Boma katika Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo.
Ripoti zinaeleza kwamba, maafa
hayo yametokana na mvua kubwa iliyonyesha wiki hii na kusababisha mto
Kalamu ufurike na kingo zake kupasuka hali iliyopelekea maji kuzagaa
katika vijiji viwili vya kusini magharibi mwa mji wa Boma. Hayo
yameelezwa na Theresa-Louise Mambu, Waziri wa Afya wa Jimbo la Kongo ya
Kati.
Aidha amewaambia waandishi wa habari
kwamba, hasara iliyosababishwa na mafuriko hayo ni kubwa mno na kuongeza
kuwa, timu ya uokozi inaendelea na kazi yake huku kukiwa na uwezekano
wa kuongezeka idadi ya vifo kutokana na watu wengi kutojulikana waliko.
Baadhi ya wakazi wa vijiji vilivyokumbwa na janga hilo la mafuriko
wanasema kuwa, wamebaki bila makazi baada ya nyumba zao kusombwa na
maji. Gavana wa Jimbo la Boma amesema kuwa, baadhi ya miili ya waliokufa
imesombwa na maji hadi nchi jirani ya Angola.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imekuwa
ikikumbwa na mafuriko mara kwa mara na kusababisha maafa makubwa. Mwaka
jana madarzeni ya watu walipoteza maisha yao mjini Kinshasa baada ya
mji huo kukumbwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua.
Wataalamu wa masuala ya hali ya hewa
wanasema kuwa, mafuriko na ukame vinatarajiwa kuongezeaka zaidi barani
Afrika kutokana na mabadiliko ya tabianchi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: