UJUMBE WA BARAZA LA USALAMA LA UN WASUBIRIWA MJINI KINSHASA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 6:12 AM
Nchini
DRC, ujumbe wa wawakilishi 15 wa nchi wanachama wa Baraza la Usalama la
Umoja wa Mataifa unatarajiwa kuwasili Ijumaa hii Novemba 11 mjini
Kinshasa hadi Novemba 14.
Lengo la
ziara hii ya siku 3 katika mji mkuu wa DRC na katika mji wa Beni
kaskazini mwa nchi ni kupunguza joto la kisiasa lililoshuhudiwa wiki za
hivi karibuni wakati ambapo unakaribia mwisho wa muhula wa pili wa
Joseph Kabila ifikapo mwezi Desemba mwaka, hasa marufuku ya kuandamana
katika mji mkuu Kinshasa na kuzimwa kwa mitambo ya RFI tangu siku 6
zilizopita.
Ujumbe wa
Baraza la Usalama Umoja wa Mataifa mjini Kinshasa, ni ishara kubwa.
Hasa katika wakati huu wa mwaka ambapo mabalozi wa Umoja wa Mataifa
hawana kawaida ya kusafiri.
Kwa
mujibu wa Umoja wa Mataifa, ni njia ya kuonyesha kuwa jumuiya ya
kimataifa inaufuatilia mgogoro wa kisiasa nchini DRC kwa umakini,
inataka ufumbuzi wa amani upatikane.
Watu
wengi wamekua wakijiuliza ni ahadi gani ujumbe huu utapata kutoka pande
husika? Hili ni tatizo kubwa kwani nchi 15 wanachama wa Baraza la
Usalama la Umoja wa Mataifa wote hawakubaliani kuhusu ujumbe
watakaowafikishia wahusika.
Kama
Marekani, Ufaransa na Uingereza watapendelea kupata ahadi kutoka kwa
Joseph Kabila kwamba hatawania katika uchaguzi wa urais, na kwamba
uchaguzi huo uahirishwe hadi mwaka 2017, nchi kama Urusi, China
wanafikiria kuwa ni kuingilia kati masuala ya ndani ya nchi iliyohuru.
Nchi hizi mbili zinataka kukaribishwa kwa makubaliano ya kisiasa
yaliyoafikiwa na kutiliwa sainimjini Kinshasa tarehe 18 Oktoba kati ya
serikali na kundi moja la vyama vya upinzani.
Kuna
uwezekano kuwa mabalozi wa Umoja wa Mataifa wakajizuia kuchukua hatua
kali na kuwataka tu wadau wote nchini DRC kushiriki uchaguzi uliyohusru
na wenye uwazi na kujiepusha na machafuko mapya kama yale yaliyotokea
mwezi Septemba uliyopita.
Jumamosi
Novemba 12, ujumbe wa Baraza la Usalama la wa Mataifa utakutana na Rais
Joseph Kabila na Waziri wa Mambo ya Nje Raymond Tshibanda. RFI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: