TANZIA

Ni baada ya muda mrefu mpendwa wetu, Fatuma  Salum kuwa katika safari huko Mozambiki katika kutafuta maisha, ametutoka Duniani akiwa katika maandalizi ya kurudi nyumbani kwao kuiona familia yake na Mzazi wake na ndugu zake waishio Kinondoni maeneo ya Mkwajuni  Jijini Dar es Salaam, ambapo siku mbili nyuma ameugua ugojwa wa kuishiwa nguvu mkono na mguu upande mmoja na kukimbizwa Hospitali na akiwa Hospitalini hapo alipata bahati ya kuongea na mama yake Mzazi na baada ya hapo tulipata taarifa ya kuwa amefariki akiwa katika maandalizi ambapo Ijumaa hii iliyopita alitarajia  aanze safari na Ijumaa hiyo hiyo mchana akaaga Dunia , hadi sasa wafanya biashara wenzake kwa kushirikiana na familia ya mpendwa wetu mwili utalala Boda na asubuhi safari itaanza, Familia ya mpendwa wetu inatowa asante kwa wote walioshiriki kufanikisha michango yao na kujinyima ili kufanikisha safari ya mpendwa kurudishwa nyumbani na wote wanao endelea kutowa pesa zao na mawazo yao. shukrani ziwafikie wafanya biasha wenzake na
Madaktari wote na ndugu na jamaa kwakufanikisha taratibu za maandalizi. (KAZI YA MUNGU)

0 comments: