TINGATINGA LA WIZARA YA ARDHI LABOMOA NYUMBA BONDE LA MKWAJUNI WILAYANI KINONDONI, DAR ES SALAAM
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:41 AM
NYUMBA na vibanda kadhaa vilivyojengwa
kwenye eneo "hatarishi" la bonde la mto Msimbazi maeneo ya Mkwajuni
jijini Dar es Salaam, zimebomolewa leo Desemba 17, 2015, baaa ya maafisa
wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makzi, wakiwa na tingatinga
kufanya kazi hiyo iliyoacha vilio kutoka kw waliokua wamiliki wa nyumba
na vibanda hivyo. Hatua hiyo inachukuliwa ikiwa ni jitihada za serikali
ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, kuchukua
tahadhari ya kujiepusha na madhara yatokanayo na mafuriko ambapo kwa
hakika eneo lote la bonde la Msimbazi takriban kila mwaka hukumbwa na
madhara makubwa yanayoambatana na vifo vya watu kutokana na mafuriklo.
Pichani Tingatinga hilo likiwa kazini
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: